Kiungo wa kimataifa wa England na timu ya Arsenal Jack Wilshere alipata majeruhi na kutolewa kwenye mchezo wa ligi kuu ya England dhidi ya Manchester United jumamosi iliyopita.
Baada ya vipimo vya madaktari imefahamika kwamba Jack Wilshare ameumia enka ya mguu na ataka nje ya uwanja kwa miezi miwili.
Majeruhi yamekuwa yakiamuandama sana kiungo huyu, hasa kwenye eneo la enka ya mguu ambayo ameshaumia mara 9, na hivyo kumsababishia kukaa nje ya uwanja kwa wiki zipatazo 112.
Hii ni sawa sawa na miaka miwili ambayo kaipoteza kwenye maisha yake ya soka kutokana na majeruhi ya enka, jambo ambalo limepelekea mashabiki wa timu pinzani kumtengenezea picha ya kiti cha kutembelea walemavu maarufu kama Wheelchair na kukiita – Wilshare
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni