MSHAMBULIAJI
Zlatan Ibrahimovic ameingia kutetea tuzo yake ya Bao Bora la Mwaka,
baada ya kutajwa katika orodha ya wanaowania tuzo ya Puskas 2014.
Mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 33 ni miongoni mwa wachezaji 10 walioingia
kwenye orodha fupi iliyoandaliwa na FIFA, fbaada ya bao lake alilofunga
dhidi ya Bastia katika Ligue 1 akiichezea klabu yake, Paris
Saint-Germain ya Ufaransa.
Msweden
huyo alishinda tuzo hiyo msimu uliopita kwa bao la umbali wa mita 30
alilofunga dhidi ya England katika ushindi wa 4-2 kwenye mchezo wa
kirafiki.
Mshindi wa Puskas 2013, Zlatan Ibrahimovic ameingia tena kuwania tuzo hiyo
Ibrahimovic
anachuana na wakali kama Diego Costa na Robin van Persie kwenye orodha
hiyo ya wachezaji 10 ya FIFA ambayo inatokana na maelfu ya mabao
yaliyofungwa kati ya Oktoba 3, mwaka 2013 hadi Septemba 26.
Mashabiki watapiga kura hadi Desemba 1 kwenye Tovuti ya FIFA ambako orodha ya wachezaji 10 itaopungua hadi kubaki watatu.
Tuzo
hizo zilizoanzishwa mwaka 2009, zikipewa heshima ya gwiji wa zamani wa
Hungary na Real Madrid, Ferenc Puskas, imekwishachukuliwa na nyota kama
Cristiano Ronaldo, Hamit Altintop, Neymar, Miroslav Stoch pamoja na
Ibrahimovic miaka iliyopita.
Ibrahimovic
alishinda tuzo hiyo mwaka jana baada ya bao aliloifungia Sweden kwa tik
tak katika ushindi wa 4-2 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya England
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni