
Nyota
huyo wa Argentina aliyeng'ara kwenye Kombe a Dunia amewasili England
huku viongozi wa Old Trafford wakiendelea na mazungumzo na Real Madrid
juu ya kukamilisha uhamisho wa dau la rekodi Uingereza.
Di
Maria, mwenye umri wa miaka 26, anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake
usiku huu ambao utamfanya alipwe Pauni 200,000 kwa wiki kwa zaidi ya
miaka mitano, mshahara ambao pia utamfanya awe mchezaji wa pili kulipwa
zaidi katika klabu hiyo baada ya Nahodha, Wayne Rooney.
Uhamisho
wote utaigharimu United zaidi ya Pauni Milioni 90 na mchezaji huyo
ataingia moja kwa moja katika kikosi kilichojeruhiwa cha Louis van Gaal
kwa ajili ya mchezo dhidi ya timu iliyopanda Ligi Kuu, Burnley.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni