KLABU
ya Manchester City imethibitisha kukamilisha usajili wa Eliaquim
Mangala kutoka Porto, na mchezaji huyo amesema anataka kushinda mataji
na mabingwa hao wa England.
Man
City ambayo inakamilisha usajili wa mchezaji huyo siku moja baada ya
kufungwa na Arsenal mabao 3-0 katika mechi ya Ngao ya Jamii, inaaminika
wamelipa Pauni Milioni 32 kumpata mchezaji huyo.
Beki
huyo wa kati atavaa jezi namba 20 Uwanja wa Etihad, na pia amesema
kusajiliwa kwa mchezaji mwenzake wa Porto, Fernando Man City kumesaidia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni