STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 16 Agosti 2014

THIBAUT COURTOIS AMSHINDA PETR CECH NA KUWA KIPA NAMBA MOJA WA JOSE MOURINHO

Rising star: Thibaut Courtois looks set to start for Chelsea against Burnley on Monday night
Nyota anayechipukia: Thibaut Courtois anatazamiwa kuanza dhidi ya Burnley.

THIBAUT Courtois ameshinda mbio za kuwa kipa namba moja wa Chelsea.
Mbelgiji huyo anatazamiwa kuanza mbele ya Petr Cech katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu jumatatu usiku dhidi ya Burnley.
Maamuzi ya Jose Mourinho kumchagua kipa huyo mwenye miaka 22 badala ya Cech ambaye amekuwa kipa namba moja kwa muongo mmoja tangu ajiunge na klabu hiyo akitokea Rennes, imeongeza mashaka juu ya hatima ya baadaye ya mchezaji huyo.
Champion: Courtois (centre) won La Liga with Atletico Madrid last season
Bingwa: Courtois (katikati) alishinda La Liga akiwa na Atletico Madrid msimu uliopita.

Paris Saint-Germain, Monaco na Real Madrid wote wanaonekana kuwa na nia ya kumsajili Cech.
Wanasubiri kuona maamuzi ya Mourinho ili kuanza harakati za kumnasa kipa huyo.
Courtois alikuwa akicheza kwa mkopo kwa misimu mitatu iliyopita katika klabu ya Atletico Madrid na alikuwa sehemu ya kikosi kilichozishangaza Real madrid na Barcelona na kutwaa ubingwa wa La Liga na kufika fainali ya UEFA.
Stalwart: Cech has been Chelsea's No 1 goalkeeper since joining the club in 2004
 Cech amekuwa kipa namba moja wa Chelsea tangu ajiunge na klabu hiyo mwaka 2004.

Mourinho anaamini atawatumia makipa wote katika kampeni zake, lakini alikiri ijumaa kwamba mchezaji asipochaguliwa kama namba moja katika kikosi chake anatakiwa kuanza kuangalia hatima yake ya baadaye klabuni hapo.
Cech mwenye miaka 32 anaweza kuamua kukaa benchi katika mechi nyingi za msimu au kutafuta ukurasa mpya wa maisha yake ya soka katika klabu nyingine

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox