Mkataba wa Chelsea na Samsung juu ya udhamini wa jezi unamalizika mwishoni mwa msimu huu.
INAFAHAMIKA
kuwa shirika la ndege la nchini Uturuki (Turkish Airlines) linapewa
nafasi kubwa ya kurithi mikoba ya udhamini wa Chelsea kutoka kwa
wadhamini wa sasa, Samsung.
Mkataba wa Samsung kudhamini jezi ya Chelsea unamalizika mwishoni mwa msimu huu.
Samsung wameidhamini Chelsea tangu mwaka 2005 chini ya Mkurugenzi mkuu wa zamani Peter Kenyon ambaye alisema klabu itaitangaza vizuri rangi ya bluu duniani.
Chelsea waliongeza mkataba wa udhamini
wa jezi yao na Samsung mwaka 2013, lakini wadau wengi wa soka
hawakufahamu sana kwasababu haikutangazwa.
Uzinduzi: Bosi wa Chelsea, Jose Mourinho (kushoto) na Mkurugenzi mkuu wa wakati huo, Peter Kenyon wakizindua udhamini mwaka 2005
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni