Rais wa Real Madrid, Florentino Perez ameitete sera ya usajili ya kalbu hiyo baada ya maoni ya Cristiano Ronaldo
RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez ameitetea sera ya klabu yake ya usajili baada ya Cristiano
Ronaldo kufunguka ya moyoni akipinga kuuzwa kwa Angel di Maria katika
klabu ya Manchester United kwa dau la paundi milioni 60.
Mabingwa hao wa Ulaya pia walimuuza
kiungo wa kimataifa wa Hispania Xabi Alonso katika klabu ya Bayern
Munich kwa dau la paundi milioni 5, kitu ambacho kimemvunja moyo Ronaldo
ambaye aliponda waziwazi maamuzi ya Perez.
Lakini Perez alisisitiza kuwa hakuna
tatizo akisema: "Namjua vizuri Cristiano Ronaldo. Cristiano ni mchezaji
bora wa dunia na mapenzi yake kwa Madrid yanajulikana".
Wametengana: Ronaldo na Angel di Maria walionesha ushirikiano mkubwa Bernabeu kabla ya mmoja kuondoka
Dili lilikamilika: Mabingwa wa Ulaya,
Real Madrid walimuuza Di Maria kwa Mancester United na kuvunja rekodi ya
usajili nchini England.
"Nimesikiliza maoni aliyosema Ronaldo na
kama ninavyomjua, kamwe haiulizi klabu. Uhusiano wangu na yeye uko
kamili, hakuna tatizo lolote. Cristiano ndiye mchezaji bora wa dunia,
hilo liko wazi"
Perez aliweka wazi kuwa Real Madrid
haikuwa na jinsi zaidi ya kumuuza Di Maria kufuatia kugoma kuongeza
mkataba ambao ungemfanya awe mchezaji wa pili kwa kulipwa vizuri katika
klabu.
"Nimekuwepo hapa tangu mwaka 2000",
Perez aliendelea."Tangu hapo wachezaji wengi wamekuja na kuondoka na
uzoefu wangu unaniambia kwamba wachezaji wengi wanaoondoka wanakuwa bora
zaidi na wanaokuja wanazua maswali"
"Usajili wangu wa kwanza ulikuwa
(Zinedine) Zidane na wa mwisho (kabla ya dirisha la majira ya kiangazi)
alikuwa (Gareth) Bale. Na tulitoa ofa nzuri kwa Di Maria na alikataa".
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni