Diego Costa ameondolewa kikosi cha Hispania baada ya kuumia nyama
MSHAMBULIAJI
wa Chelsea, Diego Costa ameondolewa kwenye kikosi cha Hispania
kitakachocheza mechi ya kuwania kufuzu kwenye fainali za Euro dhidi ya
Macedonia kutokana na maumivu ya nyama za paja.
Mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 25 alisumbuliwa na matatizo kama hayo kwa
miezi minne iliyopita na alilazimika kutolewa kwenye kikosi cha Hispania
kilichofungwa 1-0 na Ufaransa katika mchezo wa kirafiki jana baada ya
kuhisi maumivu.
Munir
El Haddadi, mchezaji mwenye thamani kubwa wa Barcelona, ataziba pengo
la Costa katika mchezo huo utakaofanyika Jumatatu mjini Valencia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni