Rio Ferdinand anaamini Man United wanaweza kujuta kumuuzaDanny Welbeck
BEKI wa zamani wa Manchester United,Rio Ferdinand amekiri kushangazwa na maamuzi ya Louis van Gaal kumuuza Danny Welbeck kwa wapinzani wao wa ligi kuu, klabu ya Arsenal.
Welbeck aliyetokea katika akademi ya
Manchester United aliuzwa Emirates siku ya mwisho ya dirisha la usajili
majira ya kiangazi kwa dau la paundi milioni 16 baada ya Van Gaal kuona
nyota huyo wa kimataifa wa England hatakuwa na namba Old Trafford.
Mkongwe huyo alisema hata kama Welbeck alifanya vizuri, Wayne Rooney na Robin Van Persiea walimfanya asionekane kitu kwa United.
Ferdinand akiongea na gazeti la The Sun
la jumapili, alizungumzia kitendo cha Welbeck kujiunga na Arsenal:
"Siamini kama United wamemruhusu Welbeck kuondoka, hususani kwenda
Arsenal. Kwa upande wangu naona ni kuchanganyikiwa".
"Ni mchezaji hatari kwa mabeiki na kama Arsenal watamtumia kiusahihi, atakuwa mtu hatari kwao"
"Nadhani hakuonekana sana United
kwasababu hata kama alifanya vizuri, Robin van Persoe na Wayne Rooney
walikuwa mbele yake. Sitashangaa kuona wanajutia kutombakisha Danny".
Mechi ijayo, Ferdinand atakutana na Man
United kwa mara ya kwanza tangu alipomaliza miaka 12 kuichezea klabu
hiyo na kujiunga na QPR.
Usajili wa mkwanja mkubwa: Welbeck alijiunga kwa mahasimu wa United, Arsenal baada ya kupewa ruhusu ya kuondoka Old Trafford
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni