Klabu ya Arsenal ndiyo inashikilia rekodi kwa tiketi zake za msimu kuwa juu, inakadiriwa kuwa ni kati ya pauni 1,014 hadi pauni 2,013 kwa msimu |
Kwa
mujibu wa ripoti liliyotelewa hivi karibuni na shirika la habari la
kimataifa BBC kupitia kitengo chake maalumu cha "BBC Sport Price of
Football", zinaonyesha kwamba, gharama za kutazama mechi za ligi kuu
nchini Uingereza kwa msimu zimepanda kwa takribani mara nne tangu mwaka
2011-2014, huku tiketi za klabu ya Arsenal za msimu zikiongoza kuwa ya
bei ya juu mno ukilinganisha na klabu zingine za nchini humo.
Inadaiwa
kwamba bei ya chini kabisa kwa sasa ya kushuhudia mechi yeyote ya siku
katika ligi zote nne za nchini Uingereza ambazo ni rasmi, ikiwemo ligi
kuu ni pauni 29 sawa na shilingi za kitanzania 58,000/= kwa kichwa.
Maana yake ni kwamba gharama hizo zimepanda kwa asilimia 13 zaidi
ukilinganisha na gharama za maisha ya kawaida nchini Uingereza ambayo
yenyewe yamepanda kwa asilimia 6.8.
Ripoti
inaonyesha kwamba tiketi za ligi kuu chini Uingereza zimepanda kwa
wastani wa pauni 508 kwa msimu zaidi ukilinganisha na za Bundesliga
(Ujerumani) ambayo wastani wake ni pauni 138 kwa mwaka. Kiwango cha
chini anacholipa shabiki wa Ujerumani kutazama mechi kwa siku husika ni
pauni 109, wakati huko Hispania ( Laliga) shabiki anaweza kupata tiketi
ya msimu kwa pauni 103 tu.
Lakini
kwa upande mwinge, ripoti hiyo pia imeonyesha kwamba, tiketi za bei ya
chini za mechi kwa siku husika (Match-day price) za klabu ya Chelsea
dimbani Stanford Bridge ni pauni 50, hali inayofanya tiketi za mechi ya
siku husika ya Chelsea kuwa ghali zaidi nchini Uingereza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni