MENEJA wa klabu ya
Arsenal, Arsene Wenger amebainisha kuwa Mesut Ozil alihisi tatizo katika
goti lake katika mchezo dhidi ya Chelsea lakini aliendelea kucheza
hivyo hivyo. Kiungo huyo alicheza dakika zote tisini katika mchezo huo
waliofungwa mabao 2-0 lakini daktari wa Ujerumani alimuondoa katika
kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kugundua kuwa kiungo huyo
amechanika msuli wa ndani la goti lake ambao unaweza kumuweka nje kwa
kipindi cha miezi mitatu. Wenger amesema anashangazwa na majeruhi ya
wachezaji wake na kukiri kuwa anapata wakati mgumu kwani inaoenekana
wachezaji wengi wenye majeruhi ya muda mrefu wameyapata bila hata
kuguswa na mchezaji mwingine. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa Ozil
alilalamika kusikia maumivu kidogo wakati wa mapumziko na alimuambia
daktari wao amuangalie na kama kutakuwa na tatizo lolote amuambie
kwasababu tayari walikuwa nyuma kwa bao moja hivyo alihitaji wachezaji
wote wa safu ya ushambuliaji. Wenger amesema kinachomshangaza ni kuwa
Ozil hakugongana na mchezaji yeyote uwanjani, alikuwa akijaribu kutoa
mpira kwa mwenzake ndipo alipoumia. Kutokana na majeruhi ya mara kwa
mara yanayoiandama klabu hiyo baadhi ya wadau wamekuwa wakihoji mazoezi
wanayopewa wachezaji hao lakini Wenger mwenyewe ametetea na kudai kuwa
ni suala la bahati mbaya kwani wachezaji wake wengi waliopata majeruhi
hivi karibuni yalitokana na wao wenyewe bila kuguswa.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 16 Oktoba 2014
WENGER ATOBOA SIRI YA MAJERUHI YA OZIL.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni