STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 16 Oktoba 2014

MESSI ATETEWA NA BABA YAKE KESI KUKWEPA KODI.

BABA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona, Lionel Messi amesisitiza kuwa mwanae huyo hahusiki na masuala yake ya kodi na hivyo hapaswi kujumuishwa katika uchunguzi wa tuhuma za ukwepaji kodi. Messi na baba yake Jorge ambao walikana tuhuma hizo wanatuhumiwa na Mamlaka ya Hispania kukwepa kulipa kodi ya kiasi cha euro milioni nne kati ya mwaka 2007 mpaka 2009. Hatua hiyo imekuja kufuatia madai kuwa mapato ya Messi katika haki za kutumia picha zake zilifichwa kwa kutumia makampuni kutoka Uruguay, Belize, Switzerland na Uingereza. Jorge amesema mara zote amekuwa akisisitiza kuwa mwanae hahusiki na suala hilo kwani ni jambo linalomhusu yeye na wakili wake analishughulikia. Messi amekuwa mkazi wa jiji la Barcelona toka mwaka 2000 na alipata uraia rasmi mwaka 2005.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox