Ni lazima usalama uwe wa hali ya juu kwa kuwa hata vyombo vilivyopo hapo uwanjani ni vya gharama ya hali ya juu
pia
|
Ni
siku ya pili sasa tangu matajiri wa Dar Azam FC watue pale jijini Mbeya
(Green City) tayari kuwakabili wenyeji Mbeya City FC "mapedeshee wa
jiji la Mbeya" siku ya Jumamosi Octoba 18, 2014 ikiwa ni mchezo wa nne
tangu ligi kuu kuanza Sep 20, 2014.
Ligi
kuu Tanzania Bara ilisimama kwa muda wa wiki moja tangu Oct 5, 2014
kupisha mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati yaTaifa Stars ya Tanzania
dhidi ya Benin, mchezo ambao ulichezwa Oct 12, 2014 na Stars kutoka
kifua mbele uwanjani baada ya kuifumua Benin kwa magoli 4-1 katika dimba
la taifa, Dar es salaam.
Kuelekea
Jumamosi ya wikiendi ijayo, Oct 18, 2014, timu sita za ligi kuu
zitashuka ugani ambapo kati ya mechi zinazotajwa kuwa na ushindani wa
hali ya juu siku hiyo ni mchezo wa Simba dhidi ya Yanga uwanja wa taifa,
halikadhalika mchezo wa Mbeya City dhidi ya Azam FC katika dimba la
kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Mbeya
City Fc hawana rekodi nzuri kwa Azam FC hususani katika dimba la
Sokoine kwa kuwa wamekuwa wakifungwa na Azam mara kwa mara
nyumbani
kwao. Kwa maana hiyo tunaamini mchezo huo utakuwa na upinzani wa hali
ya juu kwa sababu Azam naye atataka kuendeleza historia yake ya kumuonea
Mbeya City katika dimba lao la nyumbani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni