STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 17 Oktoba 2014

MOURINHO AMEAPA KUENDELEA NA TABIA YAKE YA KUTOA MKONO KWA MAKOCHA WA TIMU PINZANI KABLA YA MECHI KUMALIZIKA.


Lambert: Acha ujinga wewe, huoni muda bado?.
Baada ya wadau mbalimbali kumshambulia meneja wa Chelsea, Jose Mourihno kwa tabia yake ya kutoa mkono (kupongeza) mameneja wa timu pinzani kabla ya mechi kuisha kisha kuondoka uwanjani, Mourihno leo hii amefunguka tena na kuisitiza kuwa mtindo ni uleule (ataendelea kufanya hivyo). Mmoja kati ya watu waliomponda Mourinho na tabia yake hiyo hivi karibuni, ni kocha msaidizi wa Aston Villa na mchezaji wa zamani wa klabu ya Man U, Roy Keane. Alimbatiza Mournho kwa jina la "Mshenzi" kutokana na tabia yake hiyo.

"Kwanza napenda kusema kwamba namshukuru Keane na maoni yake, nafikiri yeye na mwenzake (Paul Lambert) ni mfano mkubwa wa watu wapole na walio elimika. Kwa sababu mimi ni mtu mstaharabu ambaye hujitahidi kujifunza kila siku, nawashukuru kwa maoni yao". Hizo ni kauli tata alizozitoa Mourinho kama kawaida yake.

Bado Mpourinho amesimamia msimamo wake kwamba hakufanyo chochote kibaya kwa Arsene Wenger katika mchezo uliopita, hivyo hana sababu ya kuomba msamaha. Lakini alipo ulizwa kuhusu msamaha aliyo ombwa hivi karibuni na Wenger, Mourinho alisema hana chochote cha kusema pia kuhusiana na hilo.

Kambla yakuibamiza Arsenal kwa magoli 2-0 siku chache zilizopita, Chelsea pia walikuwa wamesha mkung'uta Aston Villa kwa magoli 3-0 na sasa watawafuata Crystal Place kwa ajili ya mchezo wa kesho Oct 18, 2014. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox