Mshambuliaji
Javier Hernadez " "Chicharito" amesema kuendelea kukaa benchi katika
klabu ya Real Madrid kunamfanya akose furaha na kukosa kujiamini.
Mchezaji
huyo wa kimataifa wa Mexico alijiunga na mabingwa hao wa Ulaya mwanzoni
mwa msimu huu akitokea katika klabu ya Manchester United kwa mkataba wa
mkopo wa mwaka mzima.
Katika
mkataba huo Real Madrid wanakipengele cha kumsajili moja kwa moja
mshambuliaji huyo lakini hana uhakika kama ataendelea kubaki klabuni
hapo. "Ninajitahidi kwa asilimia 100 kwenye mazoezi lakini kwenye mechi
sichezi,hilo linaondoa kujiamini na ninakosa furaha" alisema Chicharito
Tangu
ajiunge na Real Madrid Chicharito amecheza mechi 13 za La Liga na
kufanikiwa kufunga magoli matatu na kutoa pasi ya mwisho moja.
Chicharito,26,
alijiunga na Real Madrid mara baada ya kukosa namba katika kikosi cha
Louis Van Gaal na pia kuwasili kwa mshabuliaji Radamel Falcao
kulichangia kwa kiasi kikubwa.
Mchezaji
huyo ambaye mkataba wake katika klabu ya Manchester United unaisha June
2016 alifunga katika mechi ya kirafiki ya juzi jumamosi ambayo
ilimalizika kwa Mexico kushinda 1-0 dhidi ya Ecuardo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni