STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 18 Machi 2015

KUTOKA KWA SALEH JEMBE: TFF ONDOENI AIBU HII, INAWAHUSU, WAPI ZINAKWENDA FEDHA ZINAZOLIPWA KWA VYAMA?

LISTI YA SIMBA VS MGAMBO...
Watu wengi hawapendi kukosolewa lakini wanaweza kuwa wavivu wa utekelezaji.

Kuna mambo mengi yanahitajika kubadilishwa katika soka la Tanzania. Huenda mengine yanaweza kuwa ya kipuuzi kabisa na hautegemei kuona yanaendelea lakini hakuna anayeyafanyia kazi.
LISTI YA BARCELONA VS MAN CITY....
Kwanini hawajayafanyii kazi? Jibu hawajali, hawaupendi mpira na wanachoangalia wao ni kuingiza fedha kutoka katika mpira. Huu ni upuuzi.
Unapokuwa jijini Dar es Salaam, mechi za Ligi Kuu Bara zimekuwa zikiandaliwa kwa mpangilio mzuri sana.
Kitu kidogo nitakupa mfano, karatasi ya listi ya wachezaji. Utaona imepangiliwa vizuri kabisa tena kwa kuchapishwa.
Lakini mechi nyingi za mkoani, karatasi zinachukuliwa zile za daftari au listi inaandikwa hovyohovyo tu. Hauwezi ukasema hii ni hadhi ya Ligi Kuu Bara.
Karatasi ya listi za wachezaji ya Ligi Kuu Bara, mechi kati ya Simba dhidi ya Mgambo haina tofauti na mechi ya mchangani. Upuuzi.
Chama cha Soka Tanzania, kinapata mgawo katika mapato ya mechi hiyo. Kununua karatasi na kufanya mambo kwa mpangilio haiwezekani?
Hakuna kiongozi anayeona hilo si sahihi, hawana aibu na wanakubali vipi ifanyike?
Kama hao wanakubali, vipi uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) nao unakubali hali hiyo? Unaona sawa kwa kuwa mambo yanakwenda?

TFF inapaswa kuwa kiongozi anayeangalia uhakika na hadhi ya inachokiongoza. Mabadiliko yafanyike. Ala!
Source... saleh jembe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox