Mshambuliaji
nyota wa Arsenal, Alexis Sanchez ameshindwa kuikoa timu yake ya taifa ya Chile
ilipokutana na kipigo cha mabao 2-0.
Chile
ilishindwa kuonyesha uwezo wa kuifunga ikiwa ni mara ya kwanza timu hizo
kukutana, mechi ikipigwa kwenye Uwanja wa NV Arena, St Polten nchini Austria.
Iran
ikiongozwa na bosi msaidizi wa zamani wa Man United, Carlos Queiroz ilionyesha
soka safi na kuwapa wakati mgumu Wachile hao.
Mabao
ya Iran katika mechi hiyo yalifungwa na
Javad
Nekounam na Vahid Amiri.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni