HUU
NDIO UJUMBE: unaweza kusema hivyo baada ya mshambuliaji wa Manchester United, Radamel
Falcao kumpelekea ujumbe kocha wake Louis van Gaal kwa vitendo.
Falcao
ambaye amekuwa akiwekwa benchi katika kikosi cha Man United, ametupia mabao
mawili ndani ya dakika nne wakati timu yake ya taifa ya Colombia ikiivaa
Bahrain katika mechi ya kirafiki.
Colombia
iliyokuwa ugenini katika mechi hiyo ya kalenda ya Fifa, ilishinda kwa mabao 6-0
huku Falcao akifunga bao la tatu na la nne ndani ya dakika nne.
Licha
ya kuwa kwao, Bahrain iliyo namba 103 kwa ubora wa Fifa, ilishindwa kufurukuta
dhidi ya Colombia iliyoonekana kuwazidi kila kitu.
Kwa
mabao hayo mawili, amefikisha mabao 55 na sasa Falcao ameshika nafasi ya pili
kwa wachezaji waliofunga mabao mengi zaidi wakiwa na kikosi cha timu ya taifa
ya Colombia.
WAFUNGAJI BORA COLOMBIA:
1
Arnoldo Iguaran 24 mabao, mechi 68
2
Radamel Falcao mabao 23 mechi 55
3
Faustino Asprilla mabao 20 mechi 57
4
Freddy Rincon mabao 17 mechi 84
5
VÃctor Aristizabal mabao 15 mechi 66
6
Teofilo Gutierrez mabao 14 mechi 37
Adolfo
Valencia mabao 14 mechi 37
8
Ivan Valenciano mabao 13 mechi 29
Antony
de Avila mabao 13 mechi 54
10
James Rodriguez mabao 12 mechi 32
Willington Jose Ortiz mabao 12 mechi 49
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni