ALEXIS Sanchez jana amekuwa mwiba mkali kwa Reading baada ya kufunga magoli mawili katika ushindi wa Arsenal wa 2-1 katika mechi ya nusu fainali ya kombe la FA.
Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya 1-1 katika dakika 90 na zikaongezwa dakika 30.
Awali Sanchez alifunga goli la kwanza dakika ya 40' lakini Garath McClearly kusawazisha dakika ya 54'.
Sanchez alifunga goli la pili dakika ya 105 na kuwapeleka Washika bunduki fainali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni