STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 20 Aprili 2015

KUTOKA MESSI NA RONALDO BASI HAZARD ANAFUATA, MOURINHO ASEMA

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema kuwa winga wa timu hiyo Eden Hazard kwa sasa anaungana na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kama moja ya kati ya wachezaji watatu bora wa kiwango cha dunia.
Hazard ambaye alifunga goli pekee katika mechi dhidi ya Man United dakika ya 38, anatazamwa na watu wengi kuwa ndiyo mchezaji atakayeinyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu nchini Uingereza (PFA).
Mourinho alisema: 'Bado ni kijana mdogo,' lakini mwenyewe anafahamu fika kuwa ni moja kati ya wachezaji bora watatu ulimwenguni, na anajitahidi sana kuendana na hali hiyo na kuitendea haki.




'Nimefanya kazi katika vilabu vingi sana, na nimekuwa na wachezaji wengi nyota, lakini huyu ana kipaji cha kipekee aisee.
'Kadiri siku zinavyokwenda anazidi kuimarika kimwili, kiakili, tena kiakili ndiyo kila siku anazidi kuimarika zaidi, anaujua vizuri sana wajibu wake, 'kabla ya mchezo dhidi ya Man United, nilimwambia kuwa:huu ni mchezo ambao hatutakiwi kabisa kupoteza.'
'Na tulihitaji kushinda ule mchezo, mwenyewe anajua fika kuwa hasa inapofikawakati timu ikiwa imezidiwa, anafahamu vizuri sana pia wakati mchezo ukiwa unahitaji mbinu nyingi ili kupata matokeo.
'Pia anafahmu vizuri tu kuwa kipaji chake ni muhimu sana kwa msaada wa timu.
kwa upande wake Hazard alisema: 'Ninaweza kusema huu ndiyo msimu bora kwagu kati ya misimu yote niliyowahi kucheza hapa. kwa uzoefu wangu nimefanikiwa kumudu vipindi vyote, vigumu na virahisi kwa timu.
'Mwaka jana nilikuwa na msimu mzuri pia, lakini kwenye baadhi ya michezo nilipotea kabisa.
'Lakini msimu huu sikumbuki hata kama kuna mchezo ambao nilipotezwa uwanjani. Ni kitu kigumu sana kuwa katika kiwango kilekile kwa takribani michezo 40 au 50, ila nashukuru maana mara kadhaa nimeweza kuwa mchezaji bora wa timu katika mechi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox