STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 21 Julai 2015

MANCHESTER WAREJEA KWA RAMOS


Manchester United wametuma ofa mpya Real Madrid wakiomba kumsajili Sergio Ramos, hii ni kwa mujibu wa Diego Torres wa gazeti la  El Pais.

Mwandishi huyo anayeishi Madrid, amedai kwamba United wameweka mezai Euro milioni 60 ili kumnasa Ramos, mshindi wa kombe la dunia 2010.

Man United wanaamini beki huyo ameshawishika kujiunga nao baada ya kutofautiana na Rais wa Real Madrid, Florentino Perez.

Tayari United walishatuma ofa mbili kumsajili Ramos, lakini Madrid walikataa zote na ofa ya sasa inaweza kuwa ya mwisho.

United na Madrid wamekuwa wakivutana juu ya usajili wa Ramosi, huku miamba ya Bernabeu ikihitaji saini ya kipa wa Old Trafford, David De Gea.

Madrid tayari wamemsajili Kiko Casilla na wameonekana kukata tamaa kumpata De Gea mpaka majira ya kiangazi mwakani, hivyo United wanaona ni wakati wa kujaribu tena kumsajili Ramos.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox