STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 18 Julai 2015

MORGAN SCHNEIDERLIN AFUNGUA AKAUNTI YA MABAO MAN UNITED

MFARANSA Morgan Schneiderlin amefungua akaunti yake ya mabao mapema tu Manchester United akiichezea kwa mara ya kwanza kabisa ikishinda 1-0 dhidi ya Club America usiku wa kuamkia leo katika ziara ya kujiandaa na msimu Marekani.

Kiungo huyo alifunga bao hilo pekee katika ushindi huo dakika ya tano tu baada ya kwenda hewani kuifuata krosi ya Juan Mata na kuidondeshea nyavuni. 

Schneiderlin, Matteo Darmian na 
Memphis Depay wote walicheza dakika zote 45 mjini Seattle, wakati Bastian Schweinsteiger pia aliichezea kwa mara ya kwanza United baada ya Louis van Gaal kubadilisha wachezaji wote 11 walioanza na kuingiza wengine kipindi cha pili.

Adnan Januzaj na Ander Herrera wote walikaribia kufunga, lakini haikuwa bahati yao na sasa United inaelekea California kucheza na San Jose Earthquakes katika mchezo mwingine kwenye ziara hiyo Jumatano.

Kikosi cha Man United kipindi cha kwanza kilikuwa; Johnstone, Darmian, Jones, Blind, Shaw, Carrick, Schneiderlin, Young, Mata, Memphis na Rooney (Nahodha).

Kipindi cha pili: Lindegaard, McNair, Smalling (Nahodha), Evans, Blackett, Lingard, Schweinsteiger, Herrera, Pereira, Januzaj na Wilson.

Club America: Club America: Gonzalez, Mares/Andrade dk46, Aguilar/Marin dk68, Sambueza (Nahodha), Goltz, Arroyo/Rivera dk68, Samudio/Colula dk68, Guemez/Guerrero dk68, Quintero/Diaz dk68, Martinez/Sanchez dk68 na Buron.

Mechi zijazo ziara ya Man United ni

Julai 22,San Jose Earthquakes [ Uwanja wa Avaya,California]

Julai 25 Barcelona [Uwanja wa Levi,California]

July 30 Paris Saint-Germain (Uwanja wa Soldier Field, Illinois)

Schneiderlin celebrates his breakthrough goal with Phil Jones and Memphis Depay as United seized the early initiative 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox