Mkurugenzi
mkuu wa Manchester United, Ed Woodward yupo mjini Barcelona, Hispania
kujaribu kufanya mazungumzo ya kumsajili Pedro kwa paundi milioni 22.
Woodward
alikwea pipa jana kwenda Catalunya kushuhudia mechi ya marudiano ya
Spanish Super Cup kati ya Barcelona na Athletic Bilbao iliyopigwa uwanja
wa Camp Nou.
Inafahamika
kwamba bosi huyo wa Old Trafford anatarajia kufikia hatua nzuri ya
kukamilisha dili hilo, huku Chelsea nao wakihusishwa kuvutiwa na nyota
huyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni