STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 21 Agosti 2015

DATA ZA MSENEGALI WA SIMBA ANAYETUA DAR ES SALAAM LEO, HIZI HAPA...






















SIMBA imeamua kukata mzizi wa fitna sasa, imeamua kusajili mshambuliaji wa ‘mauaji’ kutoka nchini Senegal.
Huyo ni Papa Amadou Niang ambaye anatarajia kutua nchini leo Ijumaa akitokea Dakar, Senegal kwa Shirika la Ndege la Kenya kwa ajili ya kumalizana na Msimbazi.


Wakala wa mchezaji huyo kutoka nchini Cameroon, alitarajia kutua nchini jana ili kumalizana na uongozi wa Simba mara mchezaji huyo atakapotua.
Taarifa za uhakika kutoka Dakar zinaeleza Simba imeomba ruhusa ya mchezaji huyo afanye mazoezi na wenzake kwa siku tatu, pia imepewa nafasi imtumie katika mechi moja ili kujiridhisha kwa kuwa awali wakala wake huyo Mcameroon, alikataa asifanye majaribio.

 














Papa ambaye imeelezwa ni ndugu wa damu wa mshambuliaji nyota wa zamani na nahodha wa Senegal, Mamadou Niang ambaye alikuwa akiisumbua Taifa Stars kila walipokutana nayo, anaelezwa kuwa mmoja wa washambuliaji wenye kasi.
Taarifa za uhakika zinaeleza Niang atawasili nchini saa 3:10 asubuhi akitokea Dakar baada ya kupitia katika miji miwili ya Abidjan, Ivory Coast na Nairobi, Kenya.
Safari yake kufika Nairobi kutoka Dakar itakuwa ya saa 10 na dakika 40 na saa 1 na dakika 25 kutoka Nairobi hadi Dar es Salaam. Maana yake atatumia saa 12 na dakika 5, kuifuata Simba ya Dar es Salaam ambayo imemwambia ‘njoo tuone’.
Moja ya sifa zake kubwa ni kuwatoka mabeki, lakini ana uwezo wa kupiga mashuti makali kwa miguu yote.
Simba imeamua kujiridhisha na sifa hizo kwa siku ilizopewa ikiwa ni pamoja na kumtumia katika mechi moja ya kirafiki halafu itachukua uamuzi kama inambakiza Dar es Salaam au arejee kwao Dakar.





























Niang amecheza soka katika nchi za Ulaya kama Kazakhstan ambako aliichezea FC Vistok na kuwa mfungaji bora.
Kabla ya hapo alikuwa mshambuliaji tegemeo wa kikosi cha FF Jaro cha Finland ambako alicheza na Mkenya, Peter Opiyo, akafanikiwa kufunga mabao saba katika mechi nne.
Alijiunga na Jaro akitokea AC Oulu ya Finland pia, baadaye alikwenda kucheza Kuwait katika Klabu ya Al Shabab ambayo baadaye ilimuuza CF Mounana ya Gabon ambayo taarifa zinaeleza mwishoni mwa msimu uliopita, alisusa kuichezea baada ya ‘kukamatwa’ na ukata na kushindwa kumlipa.















Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr, amekuwa akisisitiza anahitaji straika wa ‘kufia’ nyavuni na kama ataridhika na Msenegali huyo, basi atakuwa ametimiza kiu yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox