Lihi kuu nchini Uhispania LA-LIGA itafunguliwa rasmi siku ya leo kwa mchezo mmoja utakao chezwa Dimba la La Rosaleda kwa wenyeji Malaga kuwakaribisha Sevilla
Tayari
timu hizo zimekutana mara 30 katika michuano mbalimbali ikiwemo La Liga na Copa
del Rey na inaonekana zimekuwa na ushindani wa juu kabisa.
Sevilla
imeshinda mara 11 wakati Malaga imeshinda mara 12 na zimetoka sare 7, huku
wastani wa mabao yao ya kufunga na kufungwa ukiwa sawa kabisa.
Msimu uliopita, kila timu ikiwa
imecheza mechi zake 38 kwa timu zote 20, Sevilla ilikwama katika nafasi ya 5
ikiwa na pointi 76 huku Malaga ikiishia katika nafasi ya 9 ikiwa na pointi 50
tu.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa majira ya 19:30
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni