Manchester
United sasa wamewashiwa taa ya kijani kumsajili Pedro Rodriguez baada
ya FC Barcelona, mabingwa wapya wa Uefa Super Cup kuthibitisha kwamba
nyota huyo ameomba kuondoka.
United
bado hawajasema ofa yao, lakini wapo tayari kulipa paundi milioni 22
ili kuvunja mkataba wa sasa wa Pedro kufuatia mkurugenzi wa michezo wa
Barcelona, Roberto Fernandez kusema kwamba straika huyo mwenye miaka 28
jana alicheza mechi yake ya mwisho klabuni hapo.
Pedro
alianzia benchi kwenye mchezo wa fainali wa UEFA Super Cup na akafunga
goli la tano na la ushindi, Barca ikishinda 5-4 dhidi ya Sevilla.
Pedro akishangilia goli lake jana
Manchester United wapo tayari kulipa £22million
Kabla
ya mechi kuanza hapo jana nchini Georgia, Fernandez aliiambia
Televisheni ya Hispania: “Pedro ameniambia kwamba anataka
kuondoka.Kwasasa hakuna ofa yoyote. Dau la kuvunja mkataba wa Pedro
linazungumzika, lakini hii ni mechi yake ya mwisho”.
Manchester
City pia wanahusishwa kuiwania saini ya mshambuliaji huyo wa Hispania,
ila Louis van Gaal anapigana kumsajili kwa lengo la kuziba nafasi ya
Angel di Maria alitetimkia PSG.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni