“Tunapenda
sana Jose Mourinho kuwa kocha wa Chelsea. Ni kocha mkubwa katika
historia ya klabu yetu. Lakini sasa mashabiki wanaendelea kuchoshwa na
tabia zake.
Haiwezi kupita siku asitokeze kwenye vichwa vya magazeti kwa habari mbaya.
Tumemaliza suala la kutosalimiana na Arsene Wenger, sasa yupo kwenye bifu mpya tena.
Maamuzi ya Mourinho kumshambulia daktari wetu ni ya kipumbavu. Kumuita daktari ni mjinga, yeye ndiye mjinga zaidi.
Kwanini suala hili lisingeongelewa chumbani?
Maana ya kumshambulia Carneiro hadharani ni nini?
Mwanamke
huyo ni mtu maarufu mashabiki na wachezaji wa Chelsea. Kuendelea
kurushiana maneno kuelekea mechi yetu kubwa dhidi ya Manchester City
wikiendi hii inaleta picha mbaya zaidi.
Nikiwa shabiki wa Chelsea na Mourinho, naamini hii ni moja ya njia yake ya kucheza na akili za watu.
Hataki timu itokee kurasa za nyuma ya
magazeti kwasababu ya matokeo mabaya, anahamisha akili za nyota wake
kuelekea mechi ya Etihad.
Hili limeniudhi sana. Jose kwa mara nyingine amekosea sana ingawa haitokei mara zote.
Carneiro na Mourinho wakirushiana maneno wakati wa mechi ya Chelsea dhidi ya Swansea City
“Carneiro hataondoka Chelsea licha ya kutofautiana na Mourinho jumamosi iliyopita.”
Chelsea akiifokea timu yake ya Madaktari katika sare ya 2-2 dhidi ya Swansea
Mambo hayakuwa mchezo aisee!Mourinho alichukizwa sana
Mourinho anadai mchezaji wake Eden Hazard hakuhitaji matibabu kwasababu alikuwa amechoka tu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni