Akicheza mechi yake ya kwanza msimu wa 2015/2016, Lionel Messi hakuhitaji dakika nyingi kuwanyamazisha mashabiki duniani kote.
Nyota
huyo mwenye miaka 28, raia wa Argentina alifunga magoli mawili kwa
mipira miwili iliyokufa 'Free Kick' Barcelona ikishinda 5-4 dhidi ya
Sevilla katika mechi ya fainali ya Uefa Super Cup iliyopigwa jana.
Magoli hayo yaliyopishana kwa dakika 9 tu yaliufanya mtandao wa Twitter uwe 'busy' kupita maelezo.
Mshindi huyo mara nne wa Ballon d'Or, katika maisha yake ya soka hajawahi kufunga free kick mbili ndani ya mechi moja.
Kwa
kiwango alichoonesha nyota huyo kijana wa Barcelona, ana uwezekano
mkubwa wa kushinda tuzo binafsi ya tano ya Ballon d'Or mwezi Januari
mwakani.
Tumekukusanyia baadhi ya Tweets baada ya Messi kuandika historia ya aina yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni