Gazeti la Marca limeripoti
kwamba, Manchester United wamejumuisha jina la golikipa wao, David De
Gea katika kikosi watakachotumia kwenye michuano ya Uefa Champions
League msimu huu.
Hii ni taarifa mbaya kwa klabu ya Real Madrid ambayo wanaiwinda saini ya nyota huyo wa kimataifa wa Hispania.
De
Gea mwenye umri wa miaka 24 aliyeomba kutimkia Santiago Bernabeu,
uhamisho wake umezungumzwa sana majira haya ya kiangazi, lakini sasa
ripoti mpya kutoka Old Trafford inasema kwamba, kocha Louis van Gaal
ameiambia Real Madrid kwamba, kama inataka kumsajili inatakiwa kulipa
dau litakalovunja rekodi ya dunia la paundi milioni 32 .
Agosti
18 mwaka huu, Mashetani wekundu watacheza mechi ya kwanza ya raundi ya
mwisho ya mtoano dhidi ya Club Brugge ya Ubelgiji na wanatarajia kutuma
jina la De Gea makao makuu ya UEFA kwa ajili ya kucheza Champions
League, wakimaanisha Mhispania huyo haendi popote.
Mpaka
kufikia Jumatatu, United wanatakiwa kuongeza mchezaji mmoja katika
kikosi chao cha Uefa na itawafurahisha mashabiki wa klabu hiyo kama Van
Gaal atasajili mchezaji mpya ili ajumuishwe.
Wakati
huu dirisha la majira ya kiangazi likielekea kufungwa Septemba mosi
mwaka huu, United wamekuwa wakihusishwa kumsajili winga wa Barcelona,
Pedro Rodriguez na winga wa Benfica, Nicolas Gaitan.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni