Mlinda mlango mpya: Jenkinson akiondoa hatari langoni akiwa na jezi mpya kama golikipa
Carl
 Jenkinson, ilimlazimu kucheza kama kipa jana katika mchezo kati ya West
 Ham dhidi ya Leicester ambapo West Ham walipoteza mchezo huo kwa mabao 
2-0, mchezo uliopigwa katika dimba la Upton Park, maskani kwa West Ham. 
Wagonga
 nyundo hao walikuwa wameshamaliza idadi ya wachezaji wao wanaotakiwa 
kufanyiwa mabadiliko, na mbaya zaidi ni pale kipa wao Adrian alipopewa 
kadi nyekundu na kumlazimu kutoka nje huku wakiwa hawaruhusiwa tena 
kufanya mabadiliko.
Kipa wa West Ham Andrian akizawadiwa kadi nyekundu
Jenkinson akielekea langoni kuchukua mikoba ya Andrian
Hapo
 ndipo mchezaji wa Arsenal anayecheza kwa mkopo katika klabu hiyo 
Jenkinson, alipopelekwa langoni ili kuziba nafasi ya Andrian, na kufanya
 vema kabisa akiwa langoni hapo.
"Nilihisi
 kadi ile nyekundu ilikuwa kidogo ya kikatili, sawa alinyoosha mguu juu 
lakini ilikuwa ni kwa bahati mbaya", alisema mchezaji huyo wa timu ya 
taifa ya Uingereza U-21 baada ya mchezo.
"Ilinibidi nikakae mimi golini lakini nashukuru sikuwa na kazi kubwa sana ya kufanya maana sikupata rapsha nyingi".
 

 
 

 
 
 
 
 
 
 

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni