STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 8 Novemba 2015

MASIKINI KLOPP ALALAMA NA KUSIKITISHWA NA MASHABIKI WA LIVERPOOL,ANFIELD.........

Klopp 1
Baadhi ya mashabiki wa Liverpool jana walimuacha peke yake kocha wao Jurgen Klopp mara baada ya mlinzi wa Crystal Palace, Scot Danny kufunga goli la ushindi katika dakika ya 82 ya mchezo na kufanya matokeo kuwa 2-1.

Hicho ni kipigo cha kwanza kwa kocha Jurgen Klopp tangu atue Liverpool hivi karibuni kuchukua mikoba ya Brendan Rogders aliyetupiwa virago mwezi uliopita.

Akielezea tukio hilo mara baada ya mchezo, kocha huyo raia wa Ujerumani alisema amesikitishwa sana na kitendo hicho cha mashabiki kumkimbia na kumuacha peke yake wakati timu ikihangaika kurudisha bao, hali anayoisema kuwa alijihisi mpweke zaidi na kusikitishwa sana na tukio hilo.
Klopp 2
Klopp amewataka mashabiki kuwa wavumilivu na kwamba haipendezi kutoka uwanjani kabla ya dakika ya mwisho kwani kwenye mpira lolote linaweza kutokea na kwamba ni vizuri kuisapoti timu hadi mwisho.

Aidha katika tukio jingine, Klopp alishuhudia kuumia vibaya kwa mlinzi wake wa kati Mamadou Sakho ambaye leo atafanyiwa scan kuona ni muda gani atakua nje ya uwanja.

Klopp amesema ni heri apoteze mechi hata kwa bao 3-1 kuliko kumpoteza mchezaji kwa majeruhi, kwani kwake mchezaji ndiye muhimu zaidi kuliko matokeo.
Klopp 3

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox