STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 9 Januari 2016

BREAKING NEWS: HATIMAYE SIMBA YAPATA KOCHA MSAIDIZI MRITHI WA MATOLA


KOCHA Jackson Mayanja aliyekuwa akiifundisha Coastal Union ya jijini Tanga leo ametua Simba kuwa msaidizi wa Dylan Kerr ambaye hakupata msaidizi tangu Seleman Matola ajiuzulu.
Mayanja ametua leo mchana na kuungana na kikosi cha Simba kilichopo visiwani Zanzibar ambako kinashiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi na kesho watacheza mechi ya nusu fainali dhidi ya Mtibwa Sugar.

Habari  zinasema kuwa kocha huyo amemalizana na vigogo hao na ataanza kazi mara moja japokuwa Kerr ametaka kuangalia kwanza CV zake.
''Ametua mchana wa saa 8 na ameunganisha Zanzibar ni kocha mzuri na tunaamini kwa ushirikiano wake na Kerr timu yetu itakuwa imara zaidi, kila kitu kuhusu Mayanja kipo vizuri,'' alisema kiongozi huyo.
Kiongozi huyo amesema kesho huenda kocha huyo atakuwepo kwenye Benchi la Ufundi wakati wa mechi yao ya nusu fainali.
Mayanja amewahi kuifundisha Kagera Sugar kwa mafanikio makubwa na tangu aondoke timu hiyo imekuwa ikisuasua kwenye ligi hata Coastal Union haijafanya vizuri ingawa sababu kubwa ni za kiutawala.
 
Credit: BOIPLUS

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox