RATIBA YA KOMBE LA MAPINDUZI 2016 ZANZIBAR.
Mashabiki
mbalimbali wakiwa wamekaa mkao wa kula sasa Mashindano ya Kombe la Mapinduzi
yanatarajia kuanza kutimua vumbi siku ya kesho katika Uwanja wa Amani visiwani
Zanzibar.
Mechi
kubwa za ufunguzi katika mashindano hayo zitazikutanisha klabu ya soka ya
wanajangwani Yanga dhidi Mafunzo, wakati Mtibwa watavaana na Azam.
Klabu
ya soka ya Simba yenyewe ikiwa katika hali ya furaha kabisa baada ya ushindi wa
jana baada ya kuwatandika Ndanda bao 1-0 watakuwa katika dimba siku ya jumatatu
wakikutana na timu ya Jamuhuri huku URA wakikutana na JKU.
Michuano
hiyo ina makundi mawili pekee ambapo kundi A lina timu za Simba,Jamhuri, JKU na
URA na kundi B lina Yanga, Mtibwa, Azam na Mafunzo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni