Chanzo: Calciomercato
MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic anadaiwa kujipanga kuongeza mkataba wa mwaka mmoja na Paris Saint-Germain kabla ya hajakubali ofa ya kitita cha euro milioni 50 kutoka klabu ya Qatar, pamoja na kuwaniwa na klabu za Manchester United na Arsenal.
Chanzo: Gazzetta dello Sport
PEP Guardiola anadaiwa kutaka kuanza kibarua chake Manchester City kwa kusajili wachezaji nane ili aweze kukipangua kikosi cha kwanza cha timu hiyo huku Aymeric Laporte na John Stones wakiwepo katika orodha yake.
Chanzo: ESPN
KLABU ya Fenerbahce inadaiwa kumuwania winga wa Bayern Munich Franck Ribery kufuatia taarifa kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa anajipanga kuondoka Allianz Arena majira ya kiangazi.
Chanzo: Fichajes.net
KLABU ya Chelsea inajipanga kutoa ofa ya euro milioni 40 kwa ajili ya kiungo wa Bayern Munich Arturo Vidal huku meneja mpya Antonio Conte akidaiwa kuwa na hamu kubwa ya kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Chile.
Chanzo: Gazzetto dello Sport
MKURUGENZI wa michezo wa Juventus, Fabio Paratici anadaiwa kwenda jijini Paris Jumatano iliyopita kuwatizama nyota wa PSG Edinson Cavani, Andrien Rabiot na Javier Pastore.
Chanzo: Tuttosport
MENEJA ajaye wa Bayern Munich, Carlo Ancelotti anadaiwa kutaka kumsajili winga wa Celta Vigo Johnny Castro majira ya kiangazi.
Chanzo: Midi Libre
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni