STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 14 Julai 2016

SAMATTA ANG'ARA MICHUANO YA EUROPA,TIZAMA GOLI LAKE HAPA................

Mbwana 1

 MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amefunga bao lake la kwanza katika michuano ya Europa League usiku huu, timu yake, KRC Genk ikiilaza 2-0 Buducnost ya Montenegro Uwanja wa  Luminus Arena mjini Genk.

 
 

Katika mchezo huo wa kwanza wa Raundi ya Pili ya mchujo, Samatta alifunga bao la pili dakika ya 79, baada ya kiungo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Neeskens Kebano kufunga la kwanza kwa penalti dakika ya 16.  



Samatta amekata utepe wa mabao Europa League







































Genk sasa itatakiwa kwenda kuulinda ushindi wake katika mchezo wa marudiano Julai 21, Uwanja wa Pod Goricom mjini Podgorica ili kusonga mbele Raundi ya Tatu ya mchujo.



  Ratiba ya Raundi ya Tatu ya mchujo itapangwa leo na mechi za kwanza zitachezwa Julai 28 wakati marudiano yatakuwa Agosti 4, mwaka huu.



  Timu zitakazoshinda zitakwenda hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi, ambako sasa vigogo kama Manchester United ya England wataanzia huko.



  Kikosi cha KRC Genk kilikuwa: Bizot, Castagne, Dewaest, Kumordzi, Uronen, Ndidi, Buyens/Heynen dk73, Kebano/Karelis dk76, Bailey, Buffalo na Samatta/Trossard dk87.
  Buducnost Podgorica : Dragojevic, Vusurovic (84 'Camaj), Mitrovic, Vukcevic, Radunović, Pejakovic/Seratlic dk74 Raickovic/Janketić dk59, Hoko, Đalović, Mirkovic na Raspopovic

Inawezekana hukuweza kuliona goli lililofungwa na Samatta, hii hapa video ya goli hilo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox