Beki mkongwe wa QPR, Rio
Ferdinand amesimamishwa kuichezea timu yake mechi tatu.
Kama haitoshi Shirikisho la
Soka England limempiga faini ya pauni 25,000.
Rio ameingia kwenye mgogoro
huo baada ya kumkashifu mmoja ya mtu aliyekuwa akijibizana naye kwenye mtandao
wa kijamii wa Twitter.
Beki huyo wa zamani wa Man
United alimtaka mtu huyo kumteua mama yake ili acheze vizuri.
Ingawa aliandika Septemba
Mosi, lakini FA imeamua kuchukua uamuzi huo sasa lakini ikaeleza yuko huru
kukata rufaa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni