TIMU ya Argentina imepangwa pamoja na Uruguay katika Kundi B kwenye michuano ya Copa America mwakani, 2015.
Droo hiyo
pia
imezikutanisha Colombia na wenyeji wa Kombe la Dunia 2014, Brazil.
Michuano hiyo itakayofanyika nchini Chile, itashuhudia timu hizo mbili
za Amerika Kusini zikikutana tena kwa mara nyingine, baada ya kukutana
mara mbili hivi karibuni.
Brazil
iliitoa Colombia katika Robo Fainali ya Kombe la Dunia Julai, kabla ya
Neymar kufunga bao la ushindi katika mechi ya kirafiki baina ya mataifa
hayo mawili Septemba.
Nyota wa Barcelona, Lionel Messi ataiongoza Argentina kwenye Copa America ambako wamepangwa pamoja na Chile
Rais
wa Chile, Michelle Bachelet akiwa ameshika taji la Copa America
(kushoto), wakati Rais wa Shirikisho la Soka Uruguay (AUF), Valdez
akiliwasilisha Kombe hilo wakati upangwaji wa droo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni