STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 30 Novemba 2015

SOKA LIMEVAMIWA NA SIASA BAADA YA KIKWAZO HIKI...............

Vilabu vya nchini Russia vimepigwa marufuku rasmi kusajili mchezaji wa aina yoyote kutoka klabu za Uturuki kuanzia dirisha la usajili la mwezi January 2016.

  Katazo hilo limetolewa na serikali ya Russia katika kipindi ambacho nchi za Urusi na Uturuki zipo katika msuguano mzito wa kisiasa. 

Msuguano umetokana na ndege ya kivita ya Urusi kutunguliwa na vikosi vya Uturuki katika mpaka wa nchi hiyo na Syria Jumanne iliyopita, tukio ambalo lilichukua maisha ya rubani wakati mtu mwingine alipona na kuokolewa na wanajeshi waliokuwa katika opereshenj maalum. 

Kutokana na tukio hilo, Russian imewawekea vikwazo vya kiuchumi Uturuki, vikwazo ambavyo pia vinahusisha biashara ya usajili wa wachezaji baina ya nchi hizo mbili. 

Waziri wa michezo wa Urusi Vitaly Mutko aliiambia R-Sport news agency: “Ikiwa mtu yoyote anataka kusajili mchezaji kutoka Uturuki, hakutokua na uwezekano huo.” 

Hata hivyo, aliongeza wachezaji wenye asili ya kituruki ambao wamekuwa wakicheza Urusi hawatohusika na katazo hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox