Sergi Guardiola wa pili kushoto
Kiungo Sergi Guardiola mwenye miaka 24 amekumbwa na mkosi pale alipokuwa anasajiliwa kuichezea Fc Barcelona kutokana na posti yake katika akaunti yake ya Twita.
Siku ya Jumatatu mchezaji huyo mwenye asili ya Hispania alitakiwa kusajiliwa kuitumikia Barcelona B lakini kutokana na kuposti katika akaunti ya Twita miaka miwili iliyopita {2013} kuishabikia Real Madrid kumefanya ashindwe kusajiliwa na kuonekana ni adui wa Catalan
Mchezaji huyo alipohojiwa na moja ya chombo cha habari Hispania alisema ''ujumbe huo ulitumwa na rafiki yake ambae alitumia akaunti yake"
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni