STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 28 Desemba 2015

SAMATTA MBAGALA MPAKA BRUSSELS NCHINI UBELGIJI KISHA KUTUA MJI WA GENK..........................


Tokeo la picha la SAMATTA

HIVI karibuni timu ya TP Mazembe ya DR Congo ilikuwa nchini Japan kwenye michuano ya Kombe la Dunia kwa ngazi ya klabu, lakini haikufanya vizuri baada ya kufungwa mechi zote mbili ilizocheza. 
 


Ndani ya kikosi cha Mazembe kulikuwa na Watanzania wawili, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao walicheza mechi zote. 
 


Licha ya timu hiyo kushindwa kufanya vizuri, lakini Samatta na Ulimwengu wameweka rekodi ya kuwa Watanzania wa kwanza kucheza michuano hiyo mikubwa duniani kwa ngazi ya klabu. 


Mbali na rekodi hiyo, pia Ulimwengu na Samatta wameweka rekodi zingine, ya kwanza ni ile ya kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo hakuna Mtanzania mwingine aliyewahi kufanya hivyo, pia Samatta kuwa mfungaji bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika ni rekodi nyingine kwake binafsi. 



Watanzania hao wote wana mafanikio kwa sasa, lakini Samatta ndiye anaonekana kufanikiwa zaidi kuliko Ulimwengu.


 Samatta ambaye alizaliwa miaka 23 iliyopita jijini Dar es Salaam, alikulia maeneo ya Mbagala, Dar na maisha yake ya soka aliyaanzia hukohuko huku akiwa miongoni mwa mastaa wa kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwa sasa. 


Tokeo la picha la SAMATTA
Siku zote wanasema ukiwa na kipaji ni nadra sana kutofanikiwa kwani straika huyu aliweza kuichezea Mbagala Market kuanzia ligi za chini mpaka Ligi Kuu Bara ambayo baadaye ilikuja kujulikana kwa jina la African Lyon. 


Alichezea African Lyon kwa miaka miwili kuanzia mwaka 2008 mpaka 2010, msimu wa mwaka 2010/11 akatua Simba. 


Juhudi na kujitambua kwake, kukawafanya mabosi wa Mazembe kumuondoa ndani ya kikosi cha Simba mwaka 2011 na kumpeleka DR Congo ili aichezee timu yao ambayo yupo nayo mpaka sasa. 
 Tokeo la picha la SAMATTA

Ni wazi amecheza kwa mafanikio akiwa na Mazembe kiasi kwamba mara kwa mara maskauti wanaosaka wachezaji kutoka nchi mbalimbali wamekuwa wakipiga hodi klabuni hapo kuulizia uwezekano wa kumsajili.


Imekuwa ngumu kwa bosi wa timu hiyo, Moize Katumbi kumuachia nyota huyo, lakini hali ilivyo kwa sasa, hana budi kukubaliana na hilo na sasa yupo kwenye mazungumzo ya mwisho na mabosi wa KRC Genk ya Ubelgiji inayoshiriki ligi kuu nchini humo. 

 Tokeo la picha la GENK FC

Wakala wa mchezaji huyo, Jamal Kisongo, hivi karibuni alinukuliwa akisema wapo kwenye hatua za mwisho za kumuuza Samatta kwenye timu hiyo inayoshika nafasi ya kwanza kwenye ligi yao.


 Kwa vyovyote vile, Samatta mwakani atakuwa mchezaji wa timu hiyo ambayo wakati inaanzishwa, miaka minne mbele Samatta ndiyo alizaliwa.

 Tokeo la picha la SAMATTA

 Nyota ya Samatta inazidi kung’ara siku hadi siku baada ya hivi karibuni kutajwa kwenye orodha ya wachezaji walioingia katika fainali ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika kwa wale wanaocheza ndani ya Afrika. 


Katika tuzo hiyo, Samatta anachuana na mchezaji mwenzake wa Mazembe, Mkongo, Robert Kidiaba pamoja na Mualgeria, Boudenedjah Baghdad anayeichezea Etoile du Sahel ya Tunisia ambapo hivi karibuni aliisaidia kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika. 


Tokeo la picha la genk
Kilichobaki ni kusubiri mpaka Januari 7, mwakani siku ambayo tuzo hizo zinarajiwa kutolewa huko jijini Lagos, Nigeria ili kuona kama nyota yake itang’ara tena na kujiwekea rekodi nyingine.

 Samatta akijiunga na timu hiyo, atakuwa ni mchezaji wa tatu kutoka Afrika kuwepo katika kikosi hicho msimu huu kwani kwa sasa wapo kiungo Mghana, Bennard Kumordzi na beki Mnigeria, Onyinye Wilfred Ndidi.


 Pia kama akijiunga na timu hiyo kabla ya Januari 17, basi anaweza kuwemo katika mchezo wa upinzani mkali wakati timu hiyo itakapocheza na wapinzani wao wa jadi ambao kwa sasa wanashika nafasi ya pili, Anderlecht.

Ikumbukwe K.R.C GENK kupitia akademi yao ndipo walipo tokea kina Yannick Ferreira Carrasco (Atlético Madrid), Jelle Vossen (Club Brugge), Steven Defour (RSC Anderlecht), Christian Benteke (Liverpool FC), Thibaut Courtois (Chelsea FC), Divock Origi (Liverpool FC) na  Kevin De Bruyne (Manchester City FC).



 
 

Mara ya mwisho kwa klabu hii inayotumia uwanja wa  Cristal Arena wenye kuchukua watazamaji 21,500 kushiriki michuano ya kombe la mabingwa barani Ulaya ilikuwa ni msimu wa 2011-12 na mara ya mwisho kushiriki michuano ya Europa Ligi ni msimu wa 2013-14.

                      '' PALIPO NA NIA KUNA NJIA''

IMEANDIKWA NA 
OMARY SULTAN MDOSE KWA USHIRIKIANO NA MR'CHOI
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox