STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 10 Januari 2017

AZAM WATINGA FAINALI MBELE YA KOCHA MPYA RAIA WA ROMANIA.........





Mabingwa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, mchana huu imemtangaza, Aristica Cioaba, kuwa Kocha Mkuu wa kikosi hicho.

Cioaba, 45, raia wa Romania anakuja Azam FC kurithi mikoba ya Mhispania Zeben Hernandez, aliyesitishiwa mkataba pamoja na benchi lake zima la ufundi.

img_2311

Kocha huyo atasaidiana na makocha wazawa, Idd Nassor Cheche na Kocha wa Makipa Idd Abubakar.
 

Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu Ofisa Mtendaji Mkuu wa timu hiyo, Saad Kawemba, tayari wamefanikiwa kumpata kocha huyo na wameingia naye mkataba wa muda wa miezi sita wenye kipengele cha kuongezwa.

Alisema Cioaba ana uzoefu mkubwa wa soka la Afrika na ataiongoza Azam FC kwa kipindi hiki hadi mwishoni mwa mwa msimu, ambapo baada ya kuisha watakaa tena mezani kufanya tathimini ya mafanikio yake na wapi wanaweza kuendelea kutokana na kazi iliyofanyika.

“Bodi ya Wakurugenzi ya Azam FC inapenda wadau wote wa mpira na wapenzi na mashabiki wa Azam kwamba klabu imempata mwalimu, ambaye ndiye ataiongoza klabu kwa kipindi hiki hadi mwishoni mwa msimu.

“Kwa hiyo kwa mashabiki wetu maana yake ni kwamba tukiingia kwenye mechi inayofuata ya ligi, kocha atakuwa ameanza kazi na Cheche (Idd Nassor) atakuwa msaidizi wake na benchi lake zima alilokuwa nalo hivi sasa litaendelea,” alisema.

Kawemba aliongeza kuwa hivi sasa kocha huyo atakuwa na kikosi visiwani Zanzibar kufuatilia mwenendo wa timu ulivyo na ataendelea kutoa ushauri panapohitajika na ataanza rasmi kukaa kwenye benchi mpaka pale vibali vyake vya kufanya kazi nchini vitakapokamilika.

“Taratibu hizo zitakwenda kwa mujibu wa sheria za nchi, ambapo tutaziheshimu na kuona ya kwamba tutazifanya kwa haraka zaidi ili mwalimu aweze kupata kibali cha kufanya kazi hapa nchini, kwa hayo machache tunawaomba mashabiki wetu wawe watulivu wampe sapoti kocha na wadau wote wa mpira waone ya kwamba tumefanya jambo la kheri,” alisema.
 
WAKATI HUO;
 
BAO pekee la kiungo Frank Raymond Domayo limetosja kuipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Taifa Jang’ombe katika mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi jioni ya leo Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
 
Domayo alifunga bao hilo dakika ya 33 kwa shuti la umbali wa mita 19, baada ya kuwazidi mbinu viungo wa Taifa Jang’ombe.
 
Na kwa ushindi huo, Azam FC inakwenda fainali ambako itakutana na mshindi kati ya Simba na Yanga Ijumaa. Simba na Yanga zitamenyana kuanzia Saa 2:15 usiku wa leo katika Nusu Fainali ya pili Uwanja wa Amaan.
 
 Pamoja na kufungwa, Taifa Jang’ombe walicheza vizuri na kutengeneza nafasi, lakini bahati haikuwa yao jioni ya leo.
  Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe/Himid Mao dk46, Gardiel Michael, Aggrey Morris, Yakubu Mohammed, Stephan Mpondo/Abdallah Kheri dk79, Joseph Mahundi/Enock Atta Agyei dk75, Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, John Bocco ‘Adebayor’ na Yahya Mohammed/Shaaban Iddi dk59.
  Taifa Jang’ombe; Ahmed Suleiman, Omary Yussuf, Hassan Msabah, Abdallah Shaibu, Samir Yahya, Khatib Simai/Arafat Suleiman dk53, Adam Ibrahim, Ali Mkanga, Yahya Tumbo/ally badru dk53, Meta Apingi/Hassan Salum dk74 na Mohammed Said.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox