STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 14 Mei 2016

KESSY KAONDOKA SIMBA,JE! NANI ANAFUATA




 

MWISHONI mwa wiki iliyopita, aliyekuwa beki wa Simba, Hassan Kessy alimwaga wino wa kujiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili.

Kessy ameondoka Simba wakati ambao mashabiki wa timu hiyo bado wanamuhitaji tena zaidi ya sana.
Mashabiki wa Simba walikuwa bado wanamuhitaji Kessy kwa sababu timu yao haipo vizuri katika ushindani halafu ghafla mchezaji muhimu kama yeye anaondoka, lazima iwe anguko.

Haukuwa muda sahihi kwa Kessy kuondoka Simba, lakini jeuri ya viongozi wa klabu hiyo ndiyo umesababisha hayo yote.


Mchezaji mwenyewe alikua bado anaipenda timu yake hiyo, lakini kwa mambo aliyokua akifanyiwa akaona isiwe shida, akawaachia timu yao.

Kessy ameondoka, nani anafuata? Hilo swali lipo vichwani mwa watu wengi ambao ni wanafamilia wa soka hapa nchini.
 

 Kuna tetesi kwamba straika wao, Ibrahim Ajib naye anatakiwa na Yanga, tusubiri tuone.

Kumekuwa hakuna kauli nzuri zinazotolewa na baadhi ya viongozi kuelekea kwa wachezaji wao. 
 


Nakumbuka miezi kadhaa nyuma, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba, Zacharia Hans Poppe alisikika kwenye vyombo vya habari akisema maneno ya shombo kwa kiungo wao, Mzimbabwe, Justice Majabvi ambaye kipindi hicho alikua akidai haki yake.

Kwa uvumilivu aliokuwa nao Majabvi, akabaki na mpaka leo anaendelea kuitumikia timu hiyo iliyopoteza nafasi kwa mara nyingine tena ya kushiriki michuano ya kimataifa.

 



Huu ni msimu wa nne mfululizo Simba haijashiriki michuano ya kimtaiafa inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf), mashabiki wamekuwa wakiulaumu uongozi wa klabu yao lakini viongozi wamekuwa hawajifunzi kitu.

Wachezaji wengi wa Simba wameondoka klabuni hapo kwa mizengwe na sitashangaa kuona wengine wakiondoka siku zijazo kwa staili kama ya Kessy.

Kessy alikuwa anataka kubaki Simba, lakini alipoanza kudai maslahi zaidi, Simba kwa kuona haina ikataka kutumia ubabe wao kumlazimisha kufanya wakitakacho, Kessy akagoma, kukaanza malumbano.
 





Katika malumbano hayo, siku moja Ofisa Habari wa Simba, Hajji Manara alinukuliwa na vyombo vya habari akisema: “Kessy hata akiondoka lakini Simba itabaki. 

Simba ilikuwepo kabla yake kwani yeye ndiyo nani. Aende tu Simba si ya baba yake wala ya mama yake.”

Ni wazi inaonesha kwamba viongozi wa Simba wamekua wakitumia ubabe wao kuiendesha timu, hali hiyo ni mbaya na inaweza kuleta hali mbaya zaidi ndani ya Simba siku za usoni. Wataendelea kuboronga kwa kutojitambua.

Hakuna asiyefahamu kwamba ndani ya Simba kwa sasa hali si nzuri, na hiyo ilianza kujitokeza mara tu walipotolewa kwenye michuano ya Kombe la FA hatua ya robo fainali dhidi Coastal Union. Tumaini la kwanza la kushiriki michuano ya kimataifa likaondoka.

Baada ya hapo wakaboronga katika michezo mitatu mfululizo ya Ligi Kuu Bara na kutoka kileleni, wakawaacha Yanga wakikamata usukani na mpaka wanatangazwa kuwa mabingwa hivi karibuni.

Watu wengi wamekuwa wakiizungumzia Simba kwa lugha tofauti lakini lengo lao likiwa ni moja tu, kuwapa ushauri wa nini wanatakiwa kufanya kuondokana na hiki kinachowatokea misimu nenda rudi.

Ni hivi karibuni tu lingine limeibuka klabuni hapo, wachezaji wa kigeni waligoma wakidai mishahara yao, wakati wanagoma timu ilikuwa na safari ya kwenda Ruvuma kucheza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Majimaji.

Wachezaji wachache wakasafiri na kuwaacha wale ‘maproo’ wakiendelea na mgomo. Kesho yake wachezaji wawili kati ya hao ‘maproo’ ambao ni Vincent Angban na Majabvi, wakaungana na timu.

Wengine waliobaki ambao ni Hamisi Kiiza, Juuko Murshid, Emery Nimubona, Brian Majwega na Paul Kiongera, inasemekana hawatakiwi tena klabu hapo.
 


Najiuliza hivi kama kweli hawa wote wakiondoka, Simba itakuwa inaonekanaje siku zijazo ukiangalia kwa sasa Kiiza na Juuko wanaonekana kuibeba zaidi timu hiyo. 

Kiiza ndiye kinara wa mabao kwenye ligi kwa wachezaji wa Simba akiwa nayo 19. Juuko ndiye nguzo imara kwenye safu yao ya ulinzi.

Wakiondoka na kama hawatapatikana mbadala wao wa uhakika, naiona Simba ikimaliza ligi msimu ujao ikiwa nje ya nafasi tano za juu.

mdosejr@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox