Kipa
ambaye anatakiwa kwa hamu kubwa na Real Madrid bado ataendelea kukaa
benchi kwenye mechi ijayo dhidi ya Aston Villa kama ilivyokuwa kwenye
mchezo wa ufunguzi.
Licha
ya De Gea kusema kwamba yupo tayari kucheza kwa sasa, lakini kocha
wake, Louis Van Gaal amesema kwamba hatacheza kwenye mechi ijayo.
De
Gea atakosa hiyo safari kwasababu bado yupo kwenye hali ile ile
iliyosababisha kukosa namba mechi ya kwanza ambayo ni kutokuwa sawa
kisaikolojia.
De
Gea anahusishwa sana na kuhama klabu ya Manchester United na Kwasababu
kipindi cha usajili bado kipo, basi kipa huyo yupo kwenye tatizo hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni