STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 10 Agosti 2014

ANDY COLE APIGA MBILI DHIDI YA MAGWIJI WA BAYERN...YORKE NAYE ATUPIA PANDE SCHOLES


Bado wamo: Andrew Cole akisherehekea baada ya kuifungia Manchester United dhidi ya Bayern Munich Uwanja wa Allianz Arena

TIMU ya magwiji ya Manchester United imetoa safe ya kufungana mabao 3-3 na magwiji wenzao wa Bayern Munich Uwanja wa Allianz Arena. 
 
Mshambuliaji Andrew Cole aling'ara katika mchezo huo akifunga mabao mawili akicheza pamoja na pacha wake wa zamani, Dwight Yorke wakichezeshwa na kiungo Paul Scholes.
 
Lee Martin alimtilia Cole krosi ya chini kufunga bao la kwanza dakika ya tisa akimtungua Hans-Joerg Butt langoni mwa Bayern.
Paulo Sergio akafunga bao la kusawazisha dakika mbili baadaye, akimtesa Tomasz Kuszczak baada ya kumpeleka kipa huyo wa Poland sehemu tofuti na mpira.
Mshambuliaji wa zamani wa Brazil, Giovane Elber akaifungia bao la pili Bayern kabla ya Scholes kumsetia Yorke kuisawazishia United. Alexander Zickler akaifungia tena bao la ushindi Bayern kabla ya Cole kuwafungia Mashetani Wekundu bao la kusawazisha zikiwa zimebaki dakika saba.
Kikosi cha Manchester United kilikuwa: Kuszczak, Irwin, Johnsen, Dublin, Martin, Blomqvist, P. Neville, Scholes, Fortune, Cole na Yorke.
Bayern Munich: Butt, Babbel, Kreuzer, Kovac, Pflugler, Van Bommel, Thon, Sergio, Breitner, Zickler na Elber.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox