Man City imeshinda bao 1-0 dhidi ya Manchester
United katika mechi iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa nchini England na
duniani kote.
Mechi hiyo iliyokuwa ‘tamu’ na yenye
ushindani mkubwa imeisha kwa wenyeji hao kuibuka na ushindi huo baada ya Sergio
Aguero kufunga bao katika dakika ya 63.
Aguero raia wa Argentina aliunganisha krosh
kutoka kushoto ya Gael Clichy baada ya mabeki wa United kumsahau.
Man United licha ya kuwa pungufu baada ya
beki wake Chris Smalling kulambwa kadi nyekundu ilijitahidi kusawazisha lakini
wapi bana!
Smalling alilambwa kadi ya njano ya pili iliyozaa
nyekundu katika dakika ya 39.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni