ARSENAL
wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Liverpool Uwanja wa Emirates,
London usiku huu katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Hata
hivyo, Arsenal ilifanikiwa kupata bao lililofungwa na Aaron Ramsey
dakika ya tisa, lakini marefa wakalikataa kwa sababu alikuwa ameotea.

Kipa
Petr Cech aliokoa michomo miwili ya hatari ya Christian Benteke na
Philippe Coutinho kipindi cha kwanza, huku Olivier Giroud naye akikosa
bao la wazi.
Liverpool
wanamaliza mechi ya tatu bila kufungwa bao baada ya kushinda 1-0 mara
mbili dhidi ya Stoke City na Bournemouth katika mechi zake mbili za
awali za Ligi Kuu. 
Kikosi
cha Arsenal kilikuwa; Cech, Bellerin, Chambers, Gabriel, Monreal,
Coquelin/Oxlade-Chamberlain dk82, Ramsey, Ozil, Cazorla, Sanchez na
Giroud/Walcott dk73.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni