STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 30 Novemba 2015

NANI KATI YA HAWA WATATU KUWA MCHEZAJI BORA WA MWAKA 2015? SOMA TASMINI FUPI KUHUSU MCHAKATO HUO

Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Neymar wamechaguliwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka (Ballon d'Or 2015) kati ya wachezaji 23 waliokuwa wakiwania nafasi hiyo.

Messi ndiye mchezaji anayepewa kipaumbele na watu wengi wakiamini huenda akachukua tuzo hiyo kutokana na mafanikio aliyoyapata na timu ya Barcelona ambayo aliisadia kuchukua makombe matatu katika msimu uliopita (treble) wakati mpinzani wake Ronaldo ambaye anatetea taji lake akipewa nafasi ndogo kwenye tuzo hizo.

Endapo kama Messi akichukua tuzo hiyo kwenye sherehe zitakazo fanyika mjini Zurich mwezi January 11, 2016, hilo itakuwa tuzo yake ya 5 ya mchezaji bora wa dunia na atakuwa mchezaji wa kwanza kufanya hivyo.



Mwaka huu Messi ameungana na mchezaji mwenzake kwenye timu ya Barcelona Neymar, ambaye amefunga magoli 10 kwenye kombe la UEFA Champions League, ikiwemo bao muhimu kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Juventus kule Berlin.

Mbrazili huyo pia alishika nafasi ya tatu kwenye orodha ya wafungaji bora wa La Liga msimu uliopita akifunga magoli 22 na kwa sasa yeye ndiye anayeongoza kwa ufungaji kwenye ligi hiyo akiwa tayari ameshafunga magoli 14. 


Kwa upande wa makocha walioingia kwenye tatu bora ni Luis Enrique wa Barcelona, Pep Guardiola wa Bayern Munich na Jorge Sampaoli wa timu ya taifa ya Chile

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox