STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 2 Desemba 2015

RAIS WA NCHI ASIMAMISHA MECHI DAKIKA YA 63, AAGIZA TIMU ZIPIGIANE PENALTI...........

RAIS ABDEL AZIZ
Rais wa Mauritania, Mohamed Ould Abdel Aziz ametoa kali ya mwaka baada ya kulazimisha mechi iishe katika dakika  ya 63 na kutaka timu zipigiane mikwaju ya penalti.

Rais huyo alionekana kukerwa na uchezaji wa taratibu katika mechi ya Super Cup iliyokuwa inazikutanisha timu za FC Teyragh-Zeina na ACS Ksar na tayari zilikuwa zimefungana bao 1-1.
Mwamuzi alifikishiwa ujumbe huo ambao ulitoka kwa rais aliyekuwa jukwaani. Naye hakuwa na ujanja zaidi ya kutimiza hilo, mikwaju ya penalti ikapigwa.
Hata hivyo, suala hilo lilikuwa gumzo na kusababisha tafrani baadhi ya mashabiki wa soka wa Mauritania wakilaani uamuzi huo wa rais wa nchi yao kuingilia masuala ya soka.

Baada ya hapo, Ikulu ya Mauritania ilitoa taarifa kwa vyombo vya habari ikikanusha rais huyo kuhusika na suala hilo huku ikisisitiza ni uzushi mtupu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox