STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 15 Machi 2016

KUMBE KAMATI YA UFUNDI NDIYO INAYOWAPA KIBURI LEICESTER CITY, ASILIMIA 95% WANACHUKUA NDOO

Siri ya mafanikio ya Leicester City kufanya vizuri Ligi Kuu England msimu huu imegundulika, si nyingine bali ni baraka za Mtawa wa Kithailand!
 
Phra Prommangkalachan, mtawa wa Kibudha amekuwa akitembelea maskani ya Leicester mara kwa mara  kwa takribani miaka mitatu mfululizo, akiubariki uwanja na kuwafanya wachezaji kuwa na furaha muda wote. 
 
Hivyo anaamini kwamba safari zake za mara kwa mara zimekuwa na matokeo chanya na kuleta bahati kubwa kwa timu hiyo, na kupelekea klabu kuongoza ligi kwa pointi tano mbele ya Tottenham wanaoshikilia nafasi ya pili huku wakisaliwa na michezo nane tu kumaliza msimu. 
 
"Huwa nawaning'inizia hirizi kwenye shingo zao na kuwafanya wawe na furaha isiyo na kifani inayowapelekea kuwa na nguvu nyingi za kupambana uwanjani," alisema.
 
"Sijui kama walielewa nilichowaelezea kuhusu hilo, lakini walijua kwamba nilikuwa nikiwapa bahati 
 
 Mmiliki wa Leicester Vichai Srivaddhanaprabha inasemekana ni muumini mtiifu wa imani ya Budha  na anaamini msimu huu timu yake itatwaa ndoo ya EPL katika uwanja wa King Power ambapo mara zote helikopta huwa inatua hapo. 
 
"Alimleta mtawa kwa sababu ya kuleta baraka kwa timu, uongozi na wachezaji kwa ujumla", aliongeza

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox