
Kenya imeshuka hatua 12 nayo Tanzania ikashuka hatua 5 kwenye orodha ya viwango vya ubora wa soka ya Fifa iliyotolewa leo.
Harambee Stars wameshuka baada ya kushindwa mechi mbili za kufuzu kwa Kombe la Mataifa Bingwa Afrika na Guinea Bissau.
Taifa hilo la Afrika Magharibi limepanda hatua 45 hadi nambari 102.
Guinea Bissau waliichapa Kenya 1-0 mechi ya kwanza tarehe 23 Machi na kwenye mechi ya marudiano wakashinda tena 1-0 jijini Nairobi.
Miongoni mwa mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nambari 72, Rwanda inafuata nambari 87, Kenya nambari 115, Burundi nambari 122, Tanzania nambari 130 na Sudan Kusini nambari 155.
Orodha ya mataifa kumi bora Afrika ni kama ifuatavyo:
- Algeria
- Ivory Coast
- Ghana
- Senegal
- Misri
- Cape Verde
- Tunisia
- Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
- Guinea
- Congo
- Argentina
- Ubelgiji
- Chile
- Colombia
- Ujerumani
- Uhispania
- Brazil
- Ureno
- Uruguay
- England
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni